HALIMA VUNJABEI AELEZA SABABU YA KUKOSA MAPAMBANO NDANI YA NCHI, AWEKA WAZI MAHUSIANO YAKE


 Na Asha Mwakyonde, Dar es salaam 

"NAKOSA mapromota wa ndani ya  nchi wa kunipatia pambano  la ngumi (Boxing),nachukuliwa kwenda kucheza nje, napenda kuchezea nyumbani. Hii ni kwa  sababu mapromota wanahofu nitawatajia bei kubwa"haya ni maneno ya Bondia wa kike Halima Vunjabei.

Akizungumza na  Ihojo Media juzi jijini Dar es salaam Halima ameeleza kuwa 
changamoto inayomkabili  ni kukosa mapromota wa Tanzania wa  kumpatia mapambano na badala yake anachukuliwa kwenda kucheza nje ya nchi  na kwamba hali hiyo inatokana na mapromota hao  kuhofia kutajiwa bei kubwa ikiwa ni pamoja na kufanya upendeleo kwa bondioa wengine wa kike.

Bondia huyo ametaja sababu nyingine kuwa  hapati mapambano ya ndani ya nchi kutokana na mapromota kuangalia watu wao ambapo kila  mchezo wanacheza hao hai, hivyo anachukuliwa  na watu wa nje kwenda kucheza.

"Napenda nicheze hapa nyumbani,  Tanzania mimi ni nyumbani lakini naenda kucheza nje ya nchi sio kwa kupenda bali mapromota wa ngumi hawanipatii ridhiki nami nicheze hapa nchini na hii  ni kwa kuhofia nitawatajia bei kubwa," amesema Halima.

Halima ameongeza  sababu nyingine ya kutokupata mapambano ndani ya nchini ni kutokana na mabondia wenzake wa kike kumuogapa kucheza naye kila wanapogangiwa wanamkataa.

Kwa mjibu wa Halima madondia  wa kike wapo zaidi ya 35  hapa nchini lakini hawajiamini wanapoingia kwenye pambano.

MATARAJIO YAKE

Halima ameongeza kuwa matarajio yake ni kufika mbali zaidi kupitia mchezo huo wa ngumi.

Amefafanua kuwa mchezo huo anauchukulia kama kazi nyingine  wanazozifanya watu wengine ambayo inamuingizia kipato katika maisha yake.

MAHUSIANO

Akizungumzia mahusiano ya kimapenzi Halima ameeleza kuwa hana mahusiano ya kugandana gandana, hataki kumilikiwa anahitaji kummilika mwanaume.

"Sitaki kuwa na mahusiano ambayo hayataniweka huru, nahitaji mimi ndo nimmiliki mwanaume hata tukigombana nimwambie abebe kilicho chake aondoke, sitaki kwenda kwa mwanaume ambaye anakila kitu chake hii kwangu hapana," amesema. 

WITO WAKE MABONDIA WA KIKE

Halima amewataka mabondia wa kike
wasiogope mchezo wa ngumi kwani ni kama ilivyo michezo mingine huku akiwashauri wasiogope kukomaa sura kama baadhi ya jamii inavyosema na kwamba hakuna ukweli wowote wa suala hilo.

Amesema mchezo wa ngumi ni mzuri na nipendwa hapa nchini ambao unashika nafasi ya pili ambapo nafasi ya kwanza ni mpira wa miguu unaopendwa na watu wengi.

"Mchezo wa ngumi ni mchezo ambao naupenda, nilianza kucheza mpira wa miguu lakini  nikaona siendani nao ndio nikaingia kwenye ubondia nikafanya mazoezi nikaona mchezo huu naupenda," amesema Halima.

Halima amesema mchezo wa ngumi aliuanza tangu mwaka  2010  na kwamba mchezo huo anauchukulia Kama michezo mingine inavyotoa ajira kwa vijana.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI