WIZARA YA ELIMU YAPELEKA TIMU KUCHUNGUZA TAARIFA ZA WATOTO KULAWITIANA MKOANI KILIMANJARO


 Na Asha Mwakyonde, Dodoma

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imepeleka timu ya watu watatu mkoani Kilimanjaro ili kufuatilia taarifa ambazo zimetoka kwenye baadhi ya vyombo vya habari kuhusu Shule zinazofundisha watoto tabia mbaya za kulawitiana.

Hatua hiyo inakuja ikiwa ni siku moja baada ya baadhi ya vyombo vya habari kutoa faarifa zinazohusu wanafunzi kufundishwa kulawitiana.

Akizungumza jijini Dodoma leo Janauari 17,2023 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia  Profesa Adolf Mkenda ameeleza kuwa wizara imeshutushwa na taarifa hizo  imepeleka timu na kwamba  wanapenda timu hiyo  ihakikishe wana ukweli wote ili wizara iweze kuchukua hatua stahiki.

Prof.Mkenda ameitaja timu hiyo iliyopelekwa  kuwa ni kamishna wa elimu,Mkurugenzi wa udhibiti ubora pamoja na mwanasheria wa wizara huyo.

"Kuna taarifa ambazo zimetoka kwenye baadhi ya vyombo vya habari kuhusu Shule zinazofundisha watoto tabia mbaya za kulawitiana,tumezichukua kwa umuhimu mkubwa sana," Ameongeza.

Taenda kamishna wa elimu mwenye sio mwakilishi wake,Mkurugenzi wa udhibiti ubora mwenyewe sio mwakilishi wake pamoja na mwanasheria wa wizara aende haraka  sasa hivi wanapitia hizo Shule zilizotajwa na kujaribu kupata  ukweli wote," amesema Prof. Mkenda.

Kwa mujibu wa Waziri hiyo  tumeongea na Mkuu wa Mkoa husika kumuomba asaidiane na timu hiyo kwenda kule pamoja na kusaidia ili kama kuna sehemu yenye makosa ja jinai polisi wachujue hatua mara moja. 

Ameongeza kuwa wanatarajia walioenda wataleta taarifa kamali na kwamba wizara ipo tayari kuchukua hatua stahiki kudhibiti mambo hayo.

Prof. Mkenda amesema kwa kuwa suala hilo limetokea katika eneo  moja kunaweza kukawa na taarifa maeneo mengine hivyo Katibu Mkuu  wa wizara hiyo kesho  atatangaza namba ambayo mtu yoyote akijua kuna kitu kama hicho katika shule yoyote hapa nchini Shule za Umma, binafisi au Vyuo vyovyote anawezakupiga simu na kutoa taarifa na wizara hiyo kuweza kufuatilia kwa nchi nzima.

Amesema kuwa wanaongeza umakini wa kufuatilia mambo hayo kwa kuwa yanaweza kuchafua  Wizara ya elimu, yanaharibu vijana na kusababishia wazazi wakose imani na shule.

Prof. Mkenda amefafanua kuwa hivi karibuni waliketi kikao cha kujadili na kuanza mkakati wa kitaifa wa kuangalia namba ya kudhibiti vitendo hivyo vya kulawitiana ambayo vinatokea shuleni, nyumbani, njiani na sehemu mbalimbali hapa nchini.

Prof. Mkenda ameeleza kuwa suala hilo sio la wizara moja ni suala  mtambuka na kwamba kazi inaendelea na makatibu Wakuu watarudisha taarifa yao na watakuwa na mkakati mzuri zaidi wa utekelezaji wa kitaifa.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI