WAKUU WA UPELELEZI WA MIKOA NA WAKUU WA MADAWATI YA MAKOSA YA MTANDAO WAPIGWA MSASA

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk.Jimy Yonazi akizungumza wakati akifungua mafunzo ya makosa ya mtandao kwa Wakuu  wa upelelezi wa mikoa na Wakuu wa madawati.

Na Asha Mwakyonde, Dodoma

WIZARA ya Habari Mawasiliano na teknolojia ya Habari imetoa mafunzo ya makosa ya mtandao (cybercrime) kwa Wakuu wa upelelezi wa Mikoa na wakuu wa madawati ya makosa ya mtandao wa Mikoa lengo ikiwa ni kulinda usalama wa raia na nchi kwa ujumla kufuatia kuwepo kwa wimbi la uhalifu wa makosa ya mitandao nchini.

 Akifungua mafunzo hayo leo jijini Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dk.Jimy Yonazi amewataka Wakuu hao wa upelelezi kutumia mafunzo waliyopewa kukabiliana na masuala ya uhalifu wa kimtandao kwa kujifunza zaidi ili wawe wabobezi.


Hata hivyo amewataka Wakuu hao wa upelelezi kuhakikisha wanawalinda wananchi wote kwaajili ya usalama wao na mali zao kwa maslahi mapana ya Taifa.

Kwa upande wake,Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya  jinai nchini,Kamishna Camilius Wambura( DCI)amesema mafunzo hayo yatakuwa ni chachu kwa Jeshi la Polisi na malengo ni kila Askari awe na elimu kuhusu makosa ya mtandao ambayo kwa sasa yameshika kasi.


Awali,Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP,Joshua Mwangasa  amesema tayari wameshaanza mradi wa utekelezaji wa kanda sita za maabara za kiuchunguzi ili kupanua wigo wa kiuchunguzi nchini kwani awali walikuwa na maabara moja tu.



Post a Comment

0 Comments

TUENDELEE KUOMBA MUNGU HUKU TUKICHUKUA TAHADHARI DHIDI YA UGONJWA WA MPOX