MFUMO WA TAIFA WA RUFAA KUIMARISHA HUDUMA ZA USTAWI

Na WMJJWM, Dar-es-Salaam.

SERIKALI imeendelea na jitihada za kuimarisha Huduma za Ustawi  kwa Makundi Maalum nchini kwa kuhakikisha  kwamba mifumo ya kuwafikia na kuwahudumia ni rafiki.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawaka na Makundi Maalum Dkt. Seif Shekalaghe alipokua akifungua kikao kazi kilichoshirikisha wadau kutoka Wizara  za Kisekta na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Oktoba 30,2023, Jijini Dar Es Salaam.

Dkt. Shekalaghe ameeleza kuwa lengo la kikao hicho ni kuwapitisha wadau katika mifumo mbalimbali ya rufaa inayotumika  na  watoa Huduma za Ustawi wa Jamii  kutoka Serikalini na asasi za kiraia  ili kutoka na maazimio ya nini kifanyike baada ya kikao kazi hicho.

“Kumekua na mifumo mbalimbali ya kutolea taarifa za  Huduma za Ustawi  ambazo hutolewa  na vituo vinavyotoa huduma hizo vinavyoendeshwa na Serikali  na asasi za kiraia hali ambayo imesababisha changamoto katika ufuatiliaji na kukamilika kwa huduma,” amesema Dkt. Shekalage

Dkt. Shekalage ameendelea kusema kuwa wajumbe katika kikao kazi hicho wanatarajia kuandaa nyaraka zitakazowezesha kupatikana  kwa  mwongozo wa mifumo wa rufaa kwa Makundi Maalum, kundaliwa kwa taratibu za utendaji  za utoaji wa huduma (standard operating Procedures), kuandaa mfumo jumuishi wa rufaa wa kieletroniki, upatikanaji wa sera ya kuhifadhia takwimu za rufaa na huduma zinazotolewa kwa Makundi Maalum.

Aidha Makatibu Wakuu kutoka Wizara za kisekta kutoka Tanzania bara na Visiwani (Katibu Mkuu OR TAMISEMI, Katibu Mkuu WMJWW Zanzibar, Naibu Katibu Mkuu Mambo ya Ndani ya Nchi na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Afya) wameahidi kutoa ushirikiano  kwa Wizara katika kukamilisha uandaaji  wa mfumo huo wa Kitaifa wa Rufaa.

Kikao hicho kimeandaliwa na Wizara kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uingereza na wadau wa Maendeleo UNDP kikiwa na lengo  la kupata uelewa wa pamoja juu ya mfumo jumuishi wa Kitaifa wa rufaa.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI