UDOM YAPATA USHINDI WA KWANZA TAASISI ZA ELIMU YA JUU SABA SABA, KURUSHA SETELITI KUSAIDIA MAWASILIANO


 Na Asha Mwakyonde,Dar es Salaam 

CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM), kimepata tuzo ya mashindi wa kwanza kwa upande wa taasisi za elimu ya juu katika maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF),maarufu Saba Saba.

Pia Chuo hicho kipo katika mchakato wa kurusha Seteliti ambayo itasaidia kwenye mawasiliano.

Akizungumzia ushindi huo leo Julai13,2024 jijini Dar es Salaam katika maonesho hayo, Mkurugenzi wa Shahada za awali UDOM, Dk.Victor Marealle ambaye pia ni msimamizi wa maonesho kwenye banda la Chuo hicho amesema hiyo ni ishara ya kutambulika kwa kazi wanazozifanya kwa Chuo hicho.

Dk. Marealle ameeleza kuwa katika maonesho hayo wamekuja na bunifu mbalimbali za kitekinolojia ambazo zinafanywa na wanafunzi wao.

"Leo ni siku ya furaha sana Chuo kikuu cha Dodoma kwa kuibuka mahindi namba moja kwa upande wa Taasisi za elimu ya juu Tanzania," ameeleza Dk.Marealle.

Dk.Marealle ameongeza kuwa katika maonesho hayo wamekuja na baadhi ya bidhaa ambazo zimekuwa na maendeleo kutokana na kazi za wanafunzi hao huku akisema hiyo yote ni matunda yanayotokana na ufundishaji wao.

Amefafanua kuwa wanapowafundisha wanafunzi hao wahaishii kwenye nadharia bali wanaenda kufanya kwa vitendo ambavyo vinazalisha bidhaa hizo na kwamba hilo ni chimbuko la tafiti ambazo zinafanywa na wanafunzi hao kwa kushirikiana na wahadhiri wao.


"Tuzo hii kwa kweli kwetu ni chachu kama Chuo kikuu cha Dodoma kuzidi kupambana zaidi, si tu kuboresha bidhaa ambazo tumezileta lakini kutatua matatizo kwa ujumla ambayo yanaizunguka nchi yetu na kuendeleza tafiti mbalimbali," amesema.

Akizungumzia changamoto za vyuo vikuu vya elimu ya juu amesema kuwa vyuo hivyo vimekuwa vikipewa changamoto ambapo tafiti zake nyingi zinawekwa katika lugha ya kiingeze na kutumwa katika majarida ya nje na hazitumiki hapa nchini.

"Sisi tunakuja tofauti kidogo tunakuja na tafiti ambazo wanashirikiana na tasnia hii moja kwa moja, tunatafiti kwanza mahitaji ya ndani na nje halafu tunatengeneza programu ambazo zinakwenda kufiti tasnia inayotuzunguka," amesema.

Ameongeza kuwa hata tafiti wanazozifanya zinaendana na matokeo ya moja kwa moja kwenye Sayansi, huku akisema katika maonesho hayo wamekuja na baadhi ya bunifu ambazo wamezigeuza na kuwa bidhaa zinazoingia sokoni.

Mkurugenzi huyo wa Shahada za awali ameeleza kuwa UDOM hawataki machapisho yao, kazi za watafiti wao yaishie kwenye mashelfu ambapo wanakata zeende zikasaidie matatizo halisi katika jamii.

Dk. Dk.Marealle amewakaribisha wanafunzi waliomaliza kidato cha sita ambao wanasifa stahiki za kujiunga na programu mbalimbali huku akisema UDOM wanashahada za awali hadi za uzamivu.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI