WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUWA MGENI RASMI KONGOMANO LA NEEC






Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Rosemary Senyamule.



Katibu Mtendaji wa Baraza la  Taifa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Beng'i Issa .


Meneja wa Benki ya Stanbic Dodoma, Oppi  Igolola.

NA ASHA MWAKYONDE, DODOMA

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Kongamano la sita la uwezeshaji Wananchi kiuchumi ambalo linatarajia kufanyika Septemba 19Mwaka huu Jijini Dodoma.

 

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Rosemary Senyamule  ameyasema hayo leo Jijini Dodoma wakati  akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na kongamano hilo ambalo litahudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali.

 

“Nitoe wito kwa wananchi wa Dodoma  wajitokeze kuhudhuria katika kongamano hili ambalo litakuwa ni fursa kwao  katika masuala ya uwekezaji  na kama tunavyofahamu kwa sasa hapa makao makuu kwahiyo tujitokeze kwa wingi”amesema  Senyamule.

 

Ameiongeza Dodoma ina miradi mingi ya uwezeshaji kiuchumi ikiwamo ya ile ya kilimo cha umwakigili ambacho vijana wengi wamejiingiza katika kilimo hicho huku akisema kuwa jijini hilo ni salama kwenye uwekezaji.

 

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza hilo,Beng’i Issa ameainisha lengo la Kongamano hilo kuwa ni kuwawezesha wananchi kiuchumi  huku jopo la majadiliano la wakuu wa Mikoa litakuwepo pamoja na Wataalam.

 

Ameongeza kuwa kongamano hilo ni muhimu  na pekee ambalo nchini inaenda kukaa kujitathimi katika sera yao uwezeshashaji wananchini kiuchumi  hivyo kutakuwa na taarifa ya mwaka ya  ambayo inaonesha wananchi walivyowezeshwa.

 

“Kutakuwa na tuzo ya mjasiriamali bora,  taasisi bora za fedha, natoa fursa hii kuwakaribisha sana na tunaamini watu wengi watakuja Dodoma na kwa wale ambao hawatakuja kongamano hili

litaoneshwa mbashara,”amesema Katibu huyo mtendaji.


Kwa upanda wake Meneja wa Benki ya Stanbic Dodoma, Oppi  Igolola amesema kuwa kongamano hilo ni fursa kwao Kama benki kushiriki katika mijadala ya ya kuchanganua ni namna gani wanaweza kuwawezesha wananchi ili waweze kushiriki katika fursa za biashara na uwekezaji.

" Nalipongeza Baraza hili  kwa kuandaa jukwaa hili la kiuchumi lenye malengo ya chanya katika kuwawawezesha Watanzania kunufaika na fursa za uwekezaji na kukuza uchumi  wa Taifa letu," amesema Meneja huyo.

Ameeleza kuwa Benki ya Stanbic inaunga mkono juhudi za serikali katika kuchochea  maendeleo huku akisema hivi karibuni wanatarajia kuzindua kampeni inayolenga kuwawezesha wajasirimali kutumia fursa zitokananazo na huduma za kibenki.


Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI