![](https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjTc13Jt8X7Y6AR8yALRPmXNpxzGSlqmhtXRfBQjWUrIGXM0OBBxZge0f6xw1E0EH8EFvGlKIgqdHvergHyc9Cdbda5F3dZ2iY1POPwogDb-o6Yu_DGBk37ATho8PAVf7rI1SVgP4CWMj6QeKG58EX1_JBrEUwIiWsFay8GSPJHN1Vh3SaIOX0kB72_=s400)
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya akina mama na Uzazi kutoka Hospitali ya Taifa
Muhimbili (MHH), Dkt. Living Colman akizungumzia madhara ya kufanyiwa upasuaji.
Na Asha Mwakyonde, Dar es Salaam
KUTOKANA na ongezeko la Sayansi na Teknolojia
ya mitandao ya kijamii akina mama wamekuwa wakiingia You Tube na kuangalia namna
mama anavyojifungua. Kuumwa uchungu ni kazi ngumu ndio maana ikatwa leba hivyo
akina mama wakiangalia hasa wadada wenye ujauzito wa kwanza wakiangalia
wanaogopa kupitia maumivu aliyaona kupitia midandao ya kimaii. Kuna kuongeza
njia, mtoto anaweza akavutwa hivyo huingiwa na hofu na kuchangua njia rahisi ya
kufanyiwa upasuaji kwani muda wa kuumwa uchungu unaweza kuchukua saa 10 wakati
kufanyiwa upasuaji ni nusu saa au saa moja. Kutokana na njia hizo ndio maana
wadada wengi wanachagua upasuaji wanahisi haitakuwa na mateso kwao. Kujifungua
kwa upasuaji ni njia mojawapo ya akina mama kujifungua inayoweza kutumika kuokoa
maisha ya mama na mtoto. Njia hii inahusisha kupewa dawa ya usingizi anaweza
kupewa general maana ya jumla nusu kaputi kitaalimu General Anesthesia au
akapewa nganzi ya mgongoni Spinal Anesthesia. Katika njia hizi mbili
inayoonekana ni salama ni njia ya ganzi mgongoni zamani walikuwa wakitumia zaidi
njia ya nusu kaputi lakini ikaonekana kama ina madhara kwa mama na mtoto kwa
sababu inahusisha utaalamu zaidi. Dawa za usingizi zinaweza zikapenya moja kwa
moja kwenye kondo la mtoto kabla hajatolewa akavuta dawa hizo. Baada ya Sayansi
kuendelea ikaonekana kuna njia ya ganzi ambayo mama anachomwa mgongoni halafu
anapewa dawa ambayo inamuwekea ganzi kati ya usawa wa kitovu na kushuka chini
maana anafanyiwa upasuaji akiwa anajitambua. Ikaonekana njia hiyo ni salama
kidogo kwa mama na mtoto kwa maana haimzuru na haiingii kwa mtoto huyo. MADHARA
YA UPASUAJI Akizungumzia madhara ya upasuaji Daktari Bingwa wa Magonjwa ya akina
mama na Uzazi kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MHH), Dkt. Living Colman
anasema maumivu ya migongo hayo ni madhara tarajiwa (Side effects), mgonjwa
anaweza kuyapata baada ya kufanyiwa upasuaji kutokana na sababu mbalimbali.
Daktari huyo anasema sindano ile ya mgongoni wakati mama anawekewa inaweza
ikagusa mshipa wa fahamu na kwamba kuna aina fulani ya sindano hiyo ni nene
kidogo hivyo wakati inapenya inaweza ikaweka kovu. Anafafanua kuwa kuna madhara
ya haraka yanaweza kutokea baada ya upasuaji au ambayo ni ya muda mrefu. "Wakati
sindano inachomwa Kuna ute ute ambao upo kwenye mgongo unaotoka endapo utatoka
kwa wingi kidogo inaweza kusababisha mama akapata maumivu ya kichwa baada ya
zile siku mbili au tatu za upasuaji," anasema. Dkt. Colman anaongeza kuwa hali
kama kizungu zungu pamoja na maumivu ya migongo kwa wakati huo. Anaeleza kuwa
kuwa kuna madhara ya muda mrefu ambayo yanaweza yakakaa miaka kadhaa ni pamoja
na lile kovu ama mshipa wa fahamu ambao umeguswa inawezekana ukawa umepata ufa.
Pia daktari huyo anasema wakati wa baridi hali ya kawaida mama anaweza
kulalamika maumivu ya migongo ya hapa na pale. TIBA Dkt. Colman anabainisha kuwa
tiba yake ni pamoja na kufanya mazoezi, kupewa dawa za maumivu. WITO KWA AKINA
MAMA Daktari huyo anasema njia za kujifungua zipo za aina mbili kujifungua kwa
upasuaji na kwa njia ya kawaida. Anasema kujifungua kwa kawaida ndio njia sahihi
ambayy ni salama kama kila kitu kikienda vizuri kwa sababu kurudia katika hali
ya kawaida kunachukua kuda wa saa 24 hadi 48 au ndani ya siku saba ama nane
tofauti na njia ya upasuaji ambayo inachukua muda kidogo. " Katika hizi njia
lazima kutakuwa na sababu kwa nini mtu anafanyiwa upasuaji zinaweza kuwa ni kwa
mtoto au kwa mama lengo ni kuokoa maisha ya mama na mtoto," anaeleza Dkt.
Colman. Anafafanua sababu za mtoto mama anaweza akawa abaumwa uchungu na mtoto
huyo anapata shida ya mapigo ya moyo yanaenda vibaya inabidi afanyiwe upasuaji
ama kila kitu kipo vizuri lakini njia haifunguki. "Kuna upasuaji mwingine labda
mimba ya kwanza na hakuna sababu ya kitaalimu siyo ya mtoto wala ya mama lakini
anaomba," anasema Dkt. Colman. Anasema kwa maadili ya kidaktari mgonjwa anahaki
ya kuchagua njia ya tiba na anapo omba wanajaribu kimweleza madhara ambayo
anaweza kuyapata yakiwamo maumivu ya mgongo. Daktari hiyo anaeleza kuwa kama
mgonjwa anasisitiza anataka njia hiyo ya upasuaji kwa kuwa ni haki yake
wanamfanyia. USHAURI " Wamuachie mtalaam aamue kama kuna sahabu maalumu mtu
kufanyiwa upasuaji ikiwa hivyo madhara hayatatokea na kila kitu kitakuwa salama
kwa sahabu kila upasuaji lazima kuna sababu," anasema. Anasema katika madhara
yanayotokana na upasuaji ni pamoja na maumivu ya mgongo na kichwa. Dkt. Colman
anasema kuna vitu ambavyo wanavishauri kwa mgonjwa ndani ya muda wa saa 24 ili
kupunguza maumivu hayo. " Anatakiwa awe katika hali ya utulivu akiwa amelala
kitandani bila kunyanyua kichwa kwa muda wa saa 8 hadi 12, " anaeleza. Dkt.
Colman anasema mgonjwa wa upasuaji anapoaanza kunywa chai na maji anashauriwa
anywe maji mengi kidogo na kutokuongea mara kwa mara katika kipindi hicho.
Anasema inaweza kupunguza kidogo maumivu hasa ya kichwa.
0 Comments