![](https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjcs5pQy1vAmUwQGS0dGUjBjLUL7XsVC9pH1v7DM2dhiWIprtCv-K8pprc1hyIswekRKloxJyqTOUCZSZUWAD9n1LvRecInrJeAAoN8eoPnljKa5xhvwH4J23Pt1FBCc5A81hUYvhopmkFZJ0qTA4eEabdnaBGpgq1aRlJ8_VFo_AwpDZdFSRgRySu-=s320)
Kaimu Mkurugenzi Mkuu kutoka Mamlaka ya Udhibiti Wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA),Mhandisi Godfrey Chibulunje akizungumza na waandishi wa habari hawapo (pichani) wakati akitoa mwenendo wa bei za mafuta nchini.
Na Jasmine Shamwepu,Dodoma.
KAIMU Mkurugenzi Mkuu kutoka Mamlaka ya Udhibiti Wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Godfrey Chibulunje amesema kuna uwezekano mkubwa wa kuongezeka kwa bei za mafuta kwa mwezi Machi na Aprili 2022.
Hayo ameyasema leo jijini hapa na Kaimu Mkurugenzi huyo wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo wakati akitoa taarifa ya kuhusu mwenendo wa bei za mafuta nchini.
Amesema katika kufuatilia mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia mafuta yanaweza kupanda ifikapo Mwezi Machi na Aprili.
" Kutokana na hayo EWURA itaendelea kufutailia mwenendo huo kwa karibu ili kuishauri serikali hatua za kuchukua katika harakati za kupunguza makali ya bei za mafuta," amesema Chibulunje.
Hata hivyo akieleza bei za mafuta kwa Mwezi Februari amesema bei za rejareja za mafuta ya petroli, dezeli na mafuta ya taa yaliopelekwa bandari ya Dar es Salaam zimepungua kwa shilingi 21 kwa lita ya mafuta ya Petroli na shilingi 44 kwa lita ya mafuta ya taa, huku bei ya mafuta ya Dezeli ikiongezeka kwa shilingi 13 kwa lita.
Aidha ameeleza kwamba bei rejea kwa mafuta ya petroli na dezeli kwa mikoa ya Kaskazini Tanga, Kilimanjaro Arusha na Manyara zimepungua kwa shilingi 123 kwa lita ya petroli na shilingi 92 kwa dezeli.
"Bei za rejea za mafuta petroli na dezeli kwa Mikoa ya kusini Mtwara Lindi na Ruvuma zitaendelea kuwa zile zile zilizotangazwa katika toleo la tarehe 5 Januari 2022," Amesema Chibulunje.
0 Comments