DCEA IMEJIPANGA KUDHIBITI MIPAKA YA WAZI YA UKANDA WA BAHARI


 Na Asha Mwakyonde,Dodoma

MAMLAKA ya kupambana na Kudhibiti Dawa za kulevya Nchini (DCEA), imesema kuwa  imejipanga kudhibiti  mipaka ya wazi ikiwemo mipaka ya  baharini ambayo imeonekana kuwa changamoto kubwa inayochangia uingizwaji na  utolewaji wa dawa hizo.

Akizungumza Jijini Dodoma katika banda la Mamlaka hiyo  kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square, kutoka DCEA Dk. Christian Mbwasi   amesema  maeneo ya bahari yamekuwa changamoto kutokana na Tanzania kuwa na eneo huru na la wazi la ukanda wa bahari ambalo vyombo vya ulinzi na usalama vinashindwa kuyafikia kwa wakati mmoja kutokana na maeneo hayo kuwa makubwa.


Dk. Mbwasi  amesema kuwa licha ya changamoto hiyo Serikali imeweka mikakati mbalimbali ikiwemo , kutoe Elimu Kwa umma kuhusu madhara ya dawa hizo, kuwajengea uwezo watendaji kujua Nini tatizo kwenye jamii , pamoja na kuongeza mashirikiano na  mlaka nyingine za ulinzi.

Hata hivyo Dkt, Christian  ameiomba jamiia kutoa ushirikiano kwa kutoa Taarifa  kama kunauhalifu wa dawa za kulevya unaendelea kwenye maeneo yao huku akisiaitiza kuwa mtu yeyote atakae toa Taarifa juu ya vukundi au watu wanaojihusisha na Dawa za kulevya   atakuwa salama.

Dhima ya Mamlaka ya kudhibiti na Kupambana na Dawa za kulevya ni kudhibiti na Kupambana na Biashara haramu ya dawa hizo  na matumizi yake kupitia mikakati ya kisekta Kwa ajili ya ustawi wa Taifa

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI