Mafuru:Tumedhamiria kuweka jiji safi


Mkurugenzi wa jiji la Dodoma Joseph Mafuru akipanda mti katika Kata ya Chang'ombe.

Na Asha Mwakyonde, Dodoma

MKURUGENZI Wa jiji la Dodoma Joseph Mafuru amesema kuwa wameanza zoezi la usafi kata kwa kata lengo likiwa ni kuhakikisha jiji hilo linakuwa safi ambapo leo alishiriki kufanya usfi na kupanda miti katika Kata ya Chang'ombe.

Akizungumza mara baada ya kufanya usafi  leo Februari 5, 2022, jijini hapa amesema  wanafanya vitu viwili kwa wakati mmoja ambavyo  ni  usafi wa mazingira na kupanda miti.

Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa wameshatembea katika kata sita  za jiji la Dodoma na kwamba wanaendelea kuhamasisha jamii kufanya usafi.

"Sheria za mazingira zipo na wananchi wengi hawazifahamu kwa wale  wanaozifahamu wamekuwa hawazizingatii lakini sheria zipo na zinabana faini kubwa kwani ni kuanzia 50,000 hadi 300,000," ameongeza.

Hapa tumewasikia wananchi wa kata  hii ya Chang'ombe mtu anatoka nyumbani kwake anakuja kutupa mfuko wa Pampas katika eneo la shule sasa tunafanya vitu viwili tunatoa elimu," amesema.

Mafuru amesema wanatekeleza  sheria ya mazingira na ndio maana wanaongozana na polisi jamii pale watakapo mkuta mtu anachafua mazingira hapo hapo anachukuliwa hatua.

Mbali na hilo mkurugenzi huyo amefafanua kuwa wamesambaza miti kwenye shule zote Milioni 1.5  kama Waziri wa Nchi  Ofisi ya Makamu wa Rais  Muungano na Mazingira amesema Seleman Jafo anavyohamasisha  watoto kusimamia miti yao.

Kwa upande wake,Afisa Mazingira wa Jiji la Dodoma,Dickson Kimaro amesema wamekuwa wakiendelea na zoezi la utoaji wa elimu kuhusu uzoaji taka  ambapo kaya nyingi zimekuwa zikujitokeza kufanya usafi.

Post a Comment

0 Comments

TAARIFA ZA WASTAAFU NHIF KUHAKIKIWA MAHALI WALIPO