PROF. MKENDA SERIKALI KUWEKEZA KATIKA VYUO VYA UTALII NCHINI


 Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,Prof Adolf Mkenda akizungumza Jijini Dodoma wakati  akifunga  maonesho ya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi yaliyoanza June 7,2022 Katika uwanja wa Jamhuri.

Na Asha Mwakyonde,Dodoma

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda amesema kuwa serikali bado inahitaji kuimarisha vyuo katika sekta ya utalii na kuwekeza kwa lengo la  kuvisogeza mbele katika sekta hiyo 

Hayo ameyasema jijini Dodoma Juni 13, wakati akifunga maonyesho ya Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi amesema hayo ni maagizo ya Rais Samia suluhu Hassan katika hotuba yake ya kwanza alivyoshika dola ya kupitia sera na mitaala ya elimu, kuongeza, kuiandaa na kuweza kutoa huduma bora Kwa kwa muhitimu ili aweze kujiajiri na kuajirika.

Waziri Mkenda amesema kuwa mitaala ya shule za awali, msingi na sekondari wameshaipitia na kwamba kwa upande wa  vyuo vya kati vipo vya aina nyingi maudhui tofauti tofauti hivyo ni lazima kutekeleza maagizo ya Rais Samia kupitia mitaala hiyo kuongeza ubora, Ujuzi kuhakikisha wahitimu wanaajiriwa na wanajiajiri.

"Wizara ina kazi kubwa vyuo ni vingi maudhui mbalimbali hii kazi ya kupitia mitaala ya elimu shule za awali msing na na sekondari inaenda vizuri. Tulikusaya maoni ya upitishaji wa mitaala zaidi ya laki moja," amesema Prof. Mkenda.

Prof. Mkenda ameongeza kuwa bado wanakazi ya kuongeza ubora wa elimu hapa nchini ambapo maagizo ya Rais Samia ya kuongeza ujuzi ni mahitaji ya wazazi wa watoto wanaosoma  huku akitole mfano Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Dodoma kuwa kinafundisha ukarimu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Miradi na  Ufuatiliaji Rasilmali kutoka Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Waziri Salum
ameaema kuwa maonyesho hayo yana faida kubwa kwa Mamlaka hiyo na kwamba  inajukumu la kusimamia mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF).

Amesema mfuko huo unawapa ufadhili vijana na akina mama wa kujifunza usindikaji wa bidhaa mbalimbali pamoja na kukuza mambo ya utalii na Nishati na kuweza kujiajiri wenyewe Kwa kuwa ni  tatizo la ajira sio tu kwa Tanzania bali Afrika.

" Hapa tumekuja na wanufanika wa ufadhili wa mafunzo wa mfuko wa SDF kuna akina dada ambao wanasindika waini, kijana kutoka Lindi ambaye amekuja na matofali ya kuugandamana " Inter Lock" na huyu mama ambaye naye amekuja  na bidhaa zake alizosindika wote hawa tayari wanamasoko hapa nchini ," amesema.

Ameongeza kuwa  hao ni wachache waliofika katika maonyesho hayo kutokana na ufinyu wa maeneo   na kwamba TEA tayari imeshawapa mafunzo ya ujuzi  vijana zaidi ya 5000.

Mkurugenzi huyo amesema  Watanzania wanatakiwa kufahamu kuwa TEA ni mamlaka ya serikali hivyo inapambana kuhakikisha vijana  na akina mama wanapata  ujuzi ili kujikwamua kiuchumi.

Ameeleza kuwa vijana wengi wanaomaliza vyuo wanakimbilia kutafuta ujuzi wa  kujiajiri na kuwaajiri wenzao huku akisema kwamba anaamini katika mabadiliko ya mitaala ya Elimu watawekeza katika ujuzi.


Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI