TVA YATOA CHANJO ITAKAYOCHANJA MIFUGO ZAIDI YA 6000


 Na Asha Mwakyonde, Dodoma

MADAKTARI wa Mifugo nchini wametakiwa kuhakikisha wafugaji wanachanja mifugo yao lengo likiwa ni  kutokomeza magonjwa yanayoishambulia mifugo ikiwemo ugonjwa wa sotoka na kichaa cha mbwa.

Haya yamesemwa jijini Dodoma Disemba 5, 2022 na Mkurugenzi wa huduma za Mifugo, kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Profesa. Hezron Nonga wakati akikabidhi chanjo kwa wataalamu zilizotolewa na chama cha madaktari wa mifugo  nchini (TVA),zitakazotumika kuchanja mifugo zaidi ya elfu sita.

Amesema kuwa chama hicho kimetoa chanjo 1100 zenye thamani ya shilingi zaidi ya  milioni  tatu lengo ni kuwezesha wananchi wa Dodoma kuwa salama na kuepuka kichaa Cha mbwa pindi wanapong'atwa.

Prof. Nonga  amesema suala la chanjo ya mifugo linapaswa kuwa ajenda ili kutokomeza magonjwa ya mifugo kwa asilimia 70 mpaka ifikapo mwaka 2030
ambapo hadi sasa uchanjaji wa mbwa bado  upo chini  kwa asilimia 45.

"Tanzania kama nchi nyingine zipo kwenye ukanda wa kitropikali ambazo  zina joto la wastani zinawezesha vimelea  kustawi na kuzaliana kuna mvua na jua  kiasi unyevunyevu unaowezesha vimelea ambavyo vinaweza kusababisha maradhi kwa mifugo w kama minyoo fangasi na maradhi mengine," ameeleza Prof. Nonga.

Prof. Nonga ameeleza kuwa  Wizara ilichagua magonjwa 13 kama magonjwa ya kipaumbele  ikiwemo ya kichaa cha mbwa na kwamba mpango wa serikali ni kutomeza  ugonjwa wa sotoka ya mbuzi, kondoo pamoja na kichaa cha mbwa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha madaktari nchini TVA Profesa Esron Karimuribo amesema  wataendelea kushirikiana na serikali kwa kuzalisha chanjo ya mifugo ili kumaliza magonjwa ya mifugo.

“Tunaanza chanjo kesho kwa jiji la Dodoma pembezoni  kidogo mwa jiji la  katika maeneo ya nala mbalawala lakini pia tutakuja kutoa hadi jiji lengo likiwa ni kutokomeza kabisa kichaa cha mbwa” amesema  Karimuribo.

Naye Mwakilishi wa chama cha madaktari wa mifugo  Jumuiya ya Madola Profesa. Sharadhuli Kimera  amesema wao kama madtari wameona kuna  haja ya kuchangia kuboresha chanjo ya kichaa cha mbwa lengo ni mpaka ifikapo mwaka 2030 kuwe na maambukizi  sifuri ya kichaa cha mbwa.

“Tmekabidhi chanjo hizi 1100 za kichaa cha mbwa na magonjwa ya mapele ngozi kwakuwa sisi tunaelewa ni wapi panahitaji nguvu zaidi,"amesema Mwakilishi huyo.

Amefafanua kuwa shirika la afya za wanayama wameweka lengo la kuondoo kichaa cha mbwa cha binadamu kwa maambukizi  sifuri  na kwamba ugonjwa huo unaathiri  ngozi ya wanayama kwa dozi hizo itasaidia kutoa motisha kwa  wafuagaji kujali masilahi ya wafugaji hao.

Chanjo hiyo imezinduliwa katika tarafa za Nala na Mbalawala ambapo dozi 4000 zitatolewa kwa mbuzi na kondoo ili kuwakinga na ugonjwa wa sotoka.

Post a Comment

0 Comments

 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YANOLEWA