PROF. MKENDA: WAKUU WA SHULE BINAFISI ANGALIENI MAUDHUI YA VITABU VYA MISAADA KAMA VINA MAADILI


Na Asha Mwakyonde,Dodoma

WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa .Adolf Mkenda amewataka Wakuu wa shule binafisi kuangalia misaada ya vitabu wanavyopatiwa kama maadhui yake yana maadili.

Pia Prof. Mkenda amesema ni  kweli utandawazi  hasa masuala ya simu yamewezesha taarifa ambazo zinawashawishi watoto kwenda kufanya mambo ambayo ni mabaya na kwamba suala la malezi linaanzia nyumbani ni la mtambuka.

Waziri Mkenda ameyasema hayo leo Januari 21,2023 Jijini Dodoma katika  kikao cha Wadau wa Elimu wa Shule binafisi ambacho pia kimehudhiriwa na  viongozi wa Idara mbalimbali zilizopo chini ya Wizara hiyo amesema kama kuna watu wanafanya kampeni na kuona suala hilo lipitie shuleni kwa watoto ni lazima Shule hizo ziwekewe ulinzi.

Prof. Mkenda amesema kuwa dunia nzima  hasa nchi za Magharibi hakuna nchi inayoruhusu  mambo ya ngono kwa watoto na kuwataka Wakuu wa shule binafisi  kuangalia vitabu vyote  vimaeandikwa maudhui gani.


"Kama ni kweli kuna watu wanafanya kampeni na kuona hili suala  lipitia shuleni kwa watoto wetu ina maana shule zetu lazima ziwe na  ulinzi mkubwa sana," amesema Waziri huyo.

Ameongeza kuwa kazi ya ulinzi kwa watoto ni la  sekta nyeti  na kwamba hakuna kigugumizi katika  kulisemea suala hilo.

Prof. Mkenda amebainisha kuwa  shule zote za binafisi zina umuhimu  mkubwa kwa serikali na kwamba wanathamini mchango wa shule hizo.


Mmoja wa Wadau hao ,Naibu  Mkurugenzi wa Elimu kutoka Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Khamis Ally amewataka viongozi wa dini wa madhehebu tofauti tofauti ili kutoa y elimu ya madili ,dini kwa wanafunzi.

"Serikali iangalie suala la maadili shuleni kwani Taifa lolote ni maadili lisipokuwa na maadili linakuwa ni la hovyo," amesema Ally.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI