MSHUI: WANAWAKE TUWE CHACHU MATUMIZI YA TEKNOLOJIA


 Na Sifa Lubasi Kondoa

MWENYEKITI wa Wanawake Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoani Dodoma Fatuma   Mshui amewataka wanawake kuwa wabunifu ili kuleta mabadiliko katika matumizi ya  teknolojia kwani ni nyenzo muhimu  itakayowawezesha  kukuza biashara zao.

Alisema hayo juzi wakati wa mahojiano kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani yaliyofanyika katika wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma.

Álisema kuwa matumizi ya  teknolojia ni nyezo muhimu katika kuchochea.usawa. wa kijinsia ambao pia unachochewa  na mabadiko ya teknolojia

 "Kuna umuhimu mkubwa kwa  wanawake kuwa wabunifu katika maisha ya kila siku  katika kujifunza mabadiliko ya teknolojia, iii kukuza biashara zao" alisema.

Mshui alisema kuwa teknolojia imekuws na manufaa makubwa katika nyanja mbalimbali ikiwemo biashara

'Watu wengi wamekuwa wapata mafanikio zaidi kutokana na matumizi ya teknolojia katika kuwaongezea kipato  ndio maana  ubunifiu na mabadiliko ya teknolojiani muhimi," Álisema.

"Sisi   kama wanawake tumejitokeza sana Ili kumpa sapoti Rais Samia kwa kuwa anafanya kazi kubwa sana na kazi anaiweza,  kama wanawake tupo nyuma yake  kutoa sapoti , Rais Samia anaupiga mwingi, lazima tumuunge mkono kwani sisi ni Jeshi kubwa" alisema

Alisema juhudi kubwa zinazofanywa na Rais wa awamu ya sita zinatakiwa kuungwa mkono na wananchi  wote.

Kwa upande wake, Meneja wa TRA wilaya ya Kongwa , Sophia Boma alisema kuwa  katiika kufanikisha usawa wa kijinsia kuna  unuhimu mkubwa kwa wanawake kujifunza mambo mbalimbali kwa ajili ya ustawi wa shughuli zao za kila siku ikiwemo namna bora ya kufanya biashara

Kaulimbiu ya mwaka huu katika maadhimisho ya siku ya wanawake ni ‘Ubunifu na teknolojia kwa usawa wa kijinsia.’

Wakati wa maadhimisho hayo Mkuu wa wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema dhamira kuu ya kuadhimisha siku ya wanawake Duniani ni kutoa fursa kwa jamii kupima utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya maendeleo na uwezeshaji wa wanawake wote duniani.

"Lengo kuu la kuadhimisha siku ya wanawake Duniani ni kutoa fursa kwa jamii kupima utekelezaji wa maazimio, matamko, mikataba na itifaki mbalimbali za kikanda na  kimataifa zinazohusu masuala ya maendeleo ya jinsia na uwezeshaji wanawake.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI