TABORA YAANZA KUTOA ELIMU NA HAMASA YA CHANJO YA SURUA

Na.Elimu ya Afya kwa Umma 

Katika kukabiliana na Ugonjwa wa Surua Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais-TAMISEMI pamoja na Timu za Uendeshaji wa huduma za Afya ngazi ya Mikoa (RHMT ) na Halmashauri (CHMT ), Katika Mkoa  wa Tabora zimeanza kutoa Elimu kuhusu umuhimu wa chanjo kwa Watoto wenye Umri kuanzia miezi 9 hadi miaka 5 ili kuweza kuwakinga na maambukizi ya mlipuko wa ugonjwa wa Surua.

Elimu hiyo imetolewa katika Kata mbalimbali zilizopo Tabora mjini na Kata tatu zilizopo nje ya mji ambazo ni ,Ndevelwa ,Ifucha ,na Itonjanda ambapo lengo la zoezi hilo ni kuwafikia wananchi katika maeneo yao na kuwapa Elimu kwa kutumia magari maalumu ya kufanyia matangazo (PA).

Ikumbumkwe February 24  mwaka huu ,Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu alipokuwa akizindua zoezi la Uhamishaji wa Chanjo ya Surua Mkoani Katavi katika Halmashauri ya Mpimbwe aliagiza kutumika kwa mbinu mbalimbali zinazoshirikisha Jamii ikiwemo Kutumia Magari ya matangazo , Viongozi wa Vijiji na Vitongoji, Viongozi wa Dini na Kimila na Makundi mbalimbali kama vile waendesha bodaboda,wavuvi,wacheza ngoma na Waganga wa Tiba asili katika kutoa elimu na kuhamasisha Jamii kuwalinda Watoto dhidi ya Ugonjwa wa Surua kwa kuwapeleka kupata Chanjo.

Utolewaji wa Elimu hiyo kwa kutumia magari hayo  utawafanya wananchi wa Mkoa wa Tabora kupata mwamko wa  kupeleka watoto kupata Chanjo na hivyo kuwakinga dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa Surua.

Post a Comment

0 Comments

 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YANOLEWA