TANZANIA YATOA MASAADA KUISAIDIA NCHI YA MALAWI


 Na Asha Mwakyonde, Dodoma

SERIKALI Tanzania imetoa msaada wa huduma mbalimali  za kibinadamu zikiwamo chakula na Helkopta mbili  kuisaidia nchi ya Malawi kutokana na nchi  hiyo kupata dhoruba ya kimbunga kiitwacho Tropiki Freddy ambacho kimetokea Machi 13, mwaka huu na kusababisha vifo, kuharibu miundombinu,nyumba, mazao  na athari nyingne.

Akizungumza jijini Dodoma leo Machi 18,2023, Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ),Luteni Kanali Gaudentius Ilonda ameeleza kuwa Jeshi hilo  limepewa jukumu la kushiriki bega kwa bega kulepele msaada huo.

Luteni Kanali Ilonda amesema kufuatia jukumu hilo Mkuu wa Majaeshi  Jacob  Mkunda  ametoa maelekezo yanayoratibiwa na Mkuu wa Jeshi hilo  Luteni Jenarali Salum  Haji Othman.


Ameeleza kuwa magari  ya JWTZ  zaidi ya 37 yataondoka Dodoma muda wowote kupeleka msaada huo nchini Malawi  huku akiwataka wananchi kutokuwa na taharuki pindi wanapoyaona magari hayo.

"Baadhi ya magari yatayopelekwa  Malawi ni pamoja na  gari la wagonjwa (ambulance), karakana ya magari inayotembea (Mobile Workshop) na malori 20 makubwa yenye uzito wa tani 30, na malori  10 yenye uzito wa tani Zaidi ya 18," amesema Luteni Kanali Ilonda.

Luteni Kanali Ilonda amefafanua kuwa magari hayo yatasafirisha mahema,mablanketi, chakula  na mahitaji mengine ya kibinadamu  ambayo yametolewa na serikali ya Tanzania.

Ameongeza kuwa Tanzania  imetoa tani 1000 za unga wa mahindi ambapo kila siku zitaenda tani 90 kutoka Dodoma na tani 60 kutoka Iringa.


Post a Comment

0 Comments

 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YANOLEWA