KCU KUANZISHA SACCOS KUSAIDIA WAKULIMA


Na Asha Mwakyonde, Mbeya

CHAMA Kikuu cha ushirika cha Kagera (KCU),kimetenga  zaidi ya Sh  milioni 950 kwa ajili ya kuanzisha vyama vya  kuweka  akiba na mikopo (SACCOS), itakayowasaidia wakulima kuondokana kuuza kahawa kwa bei zisizo rasmi.

Akizingumza jijini Mbeya leo  Agosti 4, 2023, Mwenyekiti wa Bodi ya KCU Ressy Mashulano kwenye maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nane nane), ambayo yanafanyika Kitaifa mkoani hapa katika viwanja vya John Mwakangale yenye kaulimbiu isemayo 'Vijana na Wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula', wakati akitoa maelezo kwa  Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa,Gerald Kusaya alipotembelea banda chama hicho.

Mwenyekiti huyo amesema kuwa SACCOS hiyo ipo katika hatua za mwanzo na wanatarajia ifikapo mwanzoni mwa mwezi Novemba mwaka huu watakuwa tayari wameshaianzisha

Ameongeza kuwa chama hicho  kinaundwa na vyama vya msingi  142  na kina  wamachama 70,000 ambao wanazalisha kawaha aina ya robusta kwa asilimia 97 na asilimia 3 ni aina ya Arabica ngumu na kwamba wanamiradi ukiwamo wa mashamba hivyo wanaendesha shughuli zao kwa faida kubwa.

Amesema Mkoa wa Kagera ndio unaozalisha kahawa kwazaidi ya asilimia 55 nchini na kwa sasa wakulima wa zao hilo wanafuraha ambapo chama hicho kinaendesha minada ya moja kwa moja.

Ameongeza kuwa msimu uliopita wameweza kurudisha faida kwa wakulima ya Sh. Milioni 6,410,000 

Naye Meneja Mauzo nje ya nchi  wa KCU Josephat Sylvand amesema awali ilikuwa ni Sh. 1100 hadi 1500 kwa tani ambapo kwa sasa ni 2500 hadi 2600 na muda mwingine 2800 hasa kahawa aina ya Arabica.

"Kwa kipindi cha miaka miwili iliyopita ikilinganishwa na mika 15 ya nyuma  bei iliyofikiwa kwa sasa haijawahi kutokea," amesema.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa Kusaya  amekipongeza chama hicho kwa hatua nzuri za mafanikio kwa wakulima yakiwamo ya kutaka kuanzisha SACCOS.

Post a Comment

0 Comments

 MAGARI 25 YA TUME YA MADINI YAMEZINDULIWA,YATASAMBAZWA KWENYE OFISI ZA MAAFISA MADINI