VETA KWA KUSHIRIKIANA NA E4D YAWAPATI VIJANA 3,258 MAFUNZO YA UJUZI

 

Na Asha Mwakyonde, Dodoma 

JUMLA ya Vijana  3,258 wamenufaika na mafunzo katika Vituo vya veta vya Dodoma ,Manyara, Lindi,Singida Mikumi Gorowa na Dakawa  kupitia programu ya kukuza ajira na ujuzi Kwa maendeleo Afrika(E4D), ulioanza kutekelezwa mwezi mei mwaka huu.

Hayo yameelezwa Jijini Dodoma leo 22, 2023 na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Abdalah Ngodu, wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu Kongamano la ajira litakalofanyika tarehe 24 mwezi huu katika viwanja vya Nyerere square.

Amesema idadi ya Vijana hao wanatarajiwa kuwa nguvukazi yenye ujuzi kutokana na mradi huo na itatumika katika kukuza ajira kwenye miradi ya kimkakati ya uwekezaji kama bomba la mafuta na Bwawa la Nyerere.

Mkuu wa chuo cha ufundi cha  Veta Dodoma Stanslaus Ntibara ,amesema hadi kufikia tarehe 19 mwezi huu  jumla ya wanafunzi  1806  wa Mkoa wa Dodoma waliokuwa wameshahitimu mafunzo hayo.


Naye Mwakilishi Mshauri wa programu hiyo  kutoka Shirika la GOPA, Leah  Doto, amesema 
 mradi huo  unalenga kuwaandaa vijana kupata ajira kwenye uwekezaji ambao unafanyika hapa nchini na kuweza kujiajiri 

Tanzania  ni Miongoni mwa nchi sita za Afrika zinazotekeleza mradi wa stadi za ajira Kwa maendeleo Afrika inayofadhiliwa na Wizara ya Shirikisho la Ujerumani la Ushirika la kiuchumi na maendeleo (MBZ) na Shirika la ushirikiano wa maendeleo la korea (KOICA).

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI