DCEA: WATOTO WALIOACHA SHULE WABEBESHWA DAWA ZA KULEVYA

Na Asha Mwakyonde,Dodoma

WATOTO hasa walioaacha shule  na wale waliotelekezwa mitaani  wengi wanaotumika katika usafirishaji wa dawa za kulevya nchini na maeneo mbalimbali.

Pia jamii imetakiwa kuhakikisha ina wanalinda watoto ili wasishiriki katika biashara ya dawa za kulevya na kuepuka  kutumiwa katika kubeba dawa hizo.

Hayo yamesemwa jijini Dodoma  jana Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo katika  maadhimisho ya wiki ya sheria nchini wakati akizungumza na waandishi wa habari alisemai wapo kati oparesheni mbalimbali wamebaini kundi hilo la watoto ndio linatumiwa kwenye biashara hiyo.

Alisema kuwa watoto hao wanatumiwa katika biashara hiyo si rahisi kuwabaini na kwamba kupatia oparesheni wanazozifanya waliwabainia ambapo kwa sasa wanashirikiana na jeshi la polisi.

Kamishna jenerali huyo aliongeza kuwa kwa sasa wanatoa elimu Mijini,Mitaani,Vijijini na Familia kwa Familia ili kuhakikisha Wazazi wanawalea watoto wao na kutambua tabia zao mapema ili wasishiriki katika madawa ya kulevya.

"Tunaendelea kubaini mitandao ya dawa za kulevya za Heroin,Cocain na Methadone pamoja na wale wakulima wakubwa wa mashamba ya bangi na mirungi," alieleza.


Kwaupande wake Mkaguzi Msaidizi wa Polisi  Verediana Mlimba alisema kuwa wao kama jeshi la polisi wameweka mikakata mbalimbali ambayo kwa kiwango kikubwa jamii inawasaidia ni pamoja na mradi wa usalama wetu kwanza ambao umelenga zaidi watoto ambao wapo mashuleni kwanzia shule ya msingi,sekondari na vyuoni.

 Alisema lengo ni kudhibiti utoro kwani wamegundua kuwa utoro ni zao la uharifu kwani wanaojificha kwenye makorongo maeneo mbalimbali wanatekwa na vijana nakufanyiwa vitu vya kiuharifu ikiwemo  kuvutishwa bangi ,kubebeshwa ama kulawitiwa.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI