BRELA YATOA MSAADA KWA KITUO CHA WATOTO YATIMA


 Baadhi ya Watumishi wa BRELA , wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wanaolelewa katika Kituo cha Watoto Yatima AL-Zam Orphanage Center, kilichopo Mbagala Jijini Dar es Salaam.

Dar es salaam

WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), imetoa msaada wa bidhaa mbalimbali za chakula pamoja na mahitaji mengine katika kituo cha watoto  yatima kinachojulikana kwa jina la AL-Zam Orphanage Center  kilichopo Mbagala Zakhiem Wilayani Temeke, Jijini Dar es Salaam. 

Baadhi ya mahitaji yaliyotolewa ni pamoja na mafuta ya kupikia, ,sukari, unga wa sembe, mchele, maharage, nyama,  sabuni, madaftari, dawa ya meno, miswaki, pipi, na kalamu.

Afisa Leseni kutoka BRELA Bw.Koyan Abubakar  akizungumza kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu Bw. Godfrey Nyaisa ameeleza kuwa lengo kubwa ni kuwatia moyo watoto na uongozi wa kituo hicho kwa kazi kubwa wanayoifanya ili kuongeza juhudi ya kuwahudumia wahitaji ili kufikia ndoto zao.

“BRELA ni Taasisi inayosimamia Sajili za  kibiashara na Leseni, imefika katika kituo hiki kwakuwa ni sehemu ya jukumu la  Taasisi la kurejesha kwa jamii  mbali  na majumu ya msingi ya Taasisi", amesema  Bw. Koyan.

Kwa upande wake Afisa Msajili Mwandamizi,  Bw. Lugano Mwampeta amewaeleza watoto wanaolelewa katika kituo hicho baada ya kueleza ndoto zao katika moja ya nyimbo walizoimba kuwa, njia kuu ya kuzifikia ndoto zao ni kwa kufuata mafundisho wanayopatiwa na walezi wao kituoni hapo. 

“Njia kuu ya kufikia ndoto zenu ni kufuata mafundisho mnayopatiwa na walezi hapa kituoni, pia ili muweze kufikia ndoto hizo ni kufanya bidii katika masomo shuleni”, amefafanua Bw. Mwampeta.

Mkurugenzi wa kituo hicho   Bi. Zainab Said Buleta, ameishukuru BRELA kwa msaada huo ambao utawawezesha watoto hao kujikimu. 

Bibi Zainab ameongeza kuwa, kituo hicho kilianza  kwa kuwalea watoto 10 lakini hivi sasa kinalea  watoto 60 kati ya hao 35 ni wasichana  na  25 ni wavulana.

Post a Comment

0 Comments

 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YANOLEWA