WANAWAKE WACHOMELEAJI KUTOKA VETA WAUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS DK.SAMIA


 Na Asha Mwakyonde,Dodoma 

VIJANA  hasa wa kike wameshauriwa kutochagua kazi za kufanya na badala yake wafanye kutokana na fani walizojifunza bila kujali ugumu wa fani husika kwa lengo la kujikwambia kiuchimi.
 
Hayo yamesemwa jijini Dodoma katika maonyesho ya wiki ya Ubunifu 2023 na wanafunzi wahitimu  Wanawake wachomeleaji kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), kupitia Chuo Cha VETA Dodoma Hilda Mwajombe na Paulina Chuma  ambao wamejikita katika utengenezaji wa samani za kuchomelea kama vile vitanda  pamoja na utengenezaji wa majiko yanayotumia nishati kidogo ambayo yamelenga kwenye uhifadhi wa mazingira.

Wamesema  kuwa wameamua kujikita katika fani hiyo baada ya kuona fursa ya ajira kwenye eneo hilo pamoja na  kumuunga mkono Rais  Dk. Samia ambaye amonyesha ujasiri kwa namna anavyoingoza nchi.


Kwa upande wa Paulina amesema,licha ya kutengeneza samani za uchomeleaji pia wamebuni majiko yanayotumia mkaa na kuni  kidogo ili kunusuru misitu inayokatwa kwa kiasi kikubwa ili kupata nishati hizo.

“Majiko haya yanarahisisha mapishi hasa kwa taasisi kwani yanatumia nishati kidogo,lakini tumebuni jiko ambalo linapika juu na chini ,ambapo eneo la chini linatumika kama ovena,lakini jiko hili linaweza kubadilishwa na kutumia gesi,mkaa,kuni na umeme.”amesema Paulina

Aidha Paulina amesema,kama wanawake wameamua kujikita kwenye fani ya uchomeleaji baada ya kuona kuna fursa ambayo wanawake wengi wameikimbia kwa dhana potofu kwamba hiyo ni kazi ya wanaume kutokana na ugumu wake.

Ametumia nafasi hiyo kuwaasa vijana wa kike na wa kiume kutumia mafunzo wanayopata vyuoni katika kutatua changamoto katika jamii lakini pia watajipatia kipato cha kuendesha maisha yao.

Post a Comment

0 Comments

 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YANOLEWA