UDOM YASHIRIKI MRADI WA BBT KUTOA USHAURI

Na Asha Mwakyonde, Dar es salaam

CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM), kimeshiriki kikamilifu katika mradi wa Jenga Kesho iliyo Bora (BBT), ambao ni maalumu kwa vijana lengo likiwa ni kuunga  mkono jitihada zinazofanywa na  serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwenye miradi mikubwa ya kimaendeleo na ya kimkakati.

Mradi huo  wa BBT ulizinduliwa na Rais Dk. Samia Machi,2023 ambapo vijana 812 walichaguliwa kujiunga. 

Akizungumza jijini Dar es salaam jijini katika banda la chuo hicho   Naibu Makamu Mkuu wa UDOM (Mipango, Fedha na Utawala), Profesa Wineaster Anderson, katika Maonesho ya 18 Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU),ambayo yalianza Julai 17, na kuhitimishwa leo Julai 22, 2023 kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja yenye kaulimbiu isemayo 'Kukuza Ujuzi Nchini kupitia Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia kwa Uchumi Imara na Shindani', amesema wapo baadhi ya wataalam walihusika kutoa ushauri kuhusu mradi wa BBT.

Prof. Wineaster ameeleza kuwa chuo hicho kinatatua  changamoto zinazoikabili jamii  kwa 
 kinazalisha wataalam, kufanya tafiti na kuibua bunifu mbalimbali.

"Chuo kinaendelea kushirikiana na Serikali ili kufanikisha miradi mbalimbali ya kimaendeleo inafanikiwa ameeleza Prof. Wineaster.

Akizungumzia uwepo wao Katika maonesho hayo  amesema  wameyatumia kutoa elimu kwa Watanzania na kueleza  fursa zinazopatikana ikiwa ni pamoja na  machapisho mbalimbali.

Chuo hicho kina wanafunzi zaidi ya 30,000 na  kinafanya vizuri katika maeneo mbalimbali yakiwamo katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA),pamoja na kushinda mashindano  ya kitaifa na kimataifa.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI