TAEC YASHAURIWA KUFIKISHA ELIMU MADHARA YA MIONZI VIJIJINI

Na Asha Mwakyonde, Mbeya

TUME ya Nguvu ya Atomiki Tanzania (TAEC), imetakiwa kuendelea kuelimisha umma kuhusu matumizi salama ya mionzi kwa maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi hasa katika maeneo ya vijijini lengo likiwa ni kujilinda na madhara yatokanayo na mionzi hiyo.

Ushauri huo umetolewa Agosti leo 6, 2023 na Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Shamata Khamis, baada ya kutembelea banda la tume hiyo kwenye Maonesho ya Nanenane Kitaifa viwanja vya John Mwakangale, jijini Mbeya, ameeleza kuwa tume hiyo inatoa elimu hivyo hivyo ni vema ikawafikia wananchi waliopo vijijini.

"Ili kuwalinda  na mionzi wananchi waliopo maeneo ya vijijini ni vema mkaenda kutoa elimu hii mnayoitoa hapa nao wape kujua madhara yake," ameeleza.


Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TAEC, Peter Ngamilo, ameeleza kuwa  wanatumia mitandao ya kijamii kuhakikishia  wananchi na kwamba  elimu hiyo inawafikia  ikiwa ni pamoja na kufanya  vipindi vya kuelimisha kwenye vyombo vya habari mbalimbali kama redio na runinga.

"Mbali na elimu tunayoitoa hapa pia tunahakikisha wananchi wanafikiwa na elimu hii kwa kutumia mitandao ya kijamii," amesema.

"Mkuu huyo wa kitengo amebainisha kuwa endapo watabaini baadhi ya maeneo kuna mionzi iliyozidi wanawapeleka wataalam kuangalia  na kama mionzi hiyo utakuwepo wanasimamisha huduma 

Amesema kama  kama wakikuta mashine mbovu  wanasimamisha huduma hadi mashine hiyo itakapotengenezwa ndipo wataruhusu huduma iendelee.

Ameongeza kuwa baadhi ya majukumu ya Tume hiyo ni kunapima sampuli za mazingira kubaini uchafuzi wa mionzi kwenye mazingira, kupima kiwango cha mionzi kwenye minara ya simu na rada za mawasiliano, kukusanya, kusafirisha na kuhifadhi mabaki ya vyanzo vya mionzi.


Post a Comment

0 Comments

DKT. BITEKO ASISITIZA UMUHIMU WA MIFUMO THABITI YA NISHATI JADIDIFU KUKIDHI MAHITAJI YA NISHATI