WANANCHI NYANDA ZA JUU KUSINI WAMESHAURIWA KUTEMBELEA BANDA LA DCEA


 Na Asha mwakyonde, Mbeya 

MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya  (DCEA), imewashauri  wananchi wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kutembelea banda la mamlaka hiyo ili kupata elimu kuhusu madhara ya dawa za kulevya waone picha, dawa  halisi lengo likiwa ni kuweza kukabiliana na mapambano dhidi ya dawa hizo.

Akizungumza jijini hapa leo 2, 2023, katika maonesho ya Wakulima na Wafugaji (Nane nane), ambayo yanafanyika Kitaifa mkoani Mbeya katika viwanja vya John Mwakangale  yenye kaulimbiu isemayo 'Vijana na Wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula', Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kutoka DCEA, Florence Khambi  amesema kuwa uwepo wao katika maonesho hayo wananchi wanapata fursa ya kuziona dawa halisi za kulevya.

Khambi ameeleza kuwa bangi  ni uoto wa asili unaweza kuota sehemu yoyote ile, hivyo mwananchi  akiuona aweze kuung'oa na  asipo ung'oa mbegu yake ikikua na kukomaa itaweza kusambaa na kuenea katika maeneo mengine.

"Kwanini tunaonesha mmea wa bangi hapa ni kwa sababu ni uoto wa asili unaweza kuota sehemu yoyote ile, hivyo mwananchi yoyote akiuona aung'oe na asipo ung'oa mbegu yake ikikua na kukomaa itaweza kusambaa na kuenea katika maeneo mengine, tumeonesha ili mwananchi aweze kuujua hasa waliopo vijijini kwenye milima inaweza kusafirishwa na maji kwenda kwenye maeneo yao," ameeleza.

Ameongeza kuwa kuna dawa nyingine za viwandani zinasafirishwa kuingizwa nchini zikiwamo Kokeini, Heroin wananchi watapata kufahamu namna zinavyofungwa na kusafirishwa endapo watatembelea katika banda hilo.

Afisa huyo amesema wanawapatia wananchi waliotembelea katika banda la mamlaka hiyo ufahamu kuhusiana na dawa hizo hasa zinazoingizwa ili waweze kumtambua mfanyabiashara wa dawa  na wao waweze washiriki katika mapambo ya kupinga matumizi ya dawa za kulevya.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI