CHUO CHA MIPANGO CHAWAKARIBISHA WANAFUNZI KUJIUNGA ILI KUPATA UJUZI WA KUAJIRIWA NA KUJIAJIRI

Makamu Mkuu wa Chuo hicho anayeshughulikia Taaluma,Tafiti na Ushauri Elekezi Profesa Provident Dimoso ( Katikati), akifanya kipindi na moja ya kituo cha redio nchini alipotembelea banda la Chuo Cha Mipango lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha na Mipango kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF).

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dk. Jim Yonazi, akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Chuo Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), katika Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF).

Na Asha Mwakyonde, Dar es salaam 

TAKWIMU  zinaonesha umasikini mwingi upo vijijini na moja ya utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP),
 ilionekana moja ya sababu inayochangia umasikini wa wananchi ni  kutegemea shughuli ya kilimo kwa kiwango kikubwa zaidi kuliko nyingine.

Pia Chuo hicho kinawakaribisha wanafunzi kujiunga  kwani ufundishaji wake ni wa vitendo na nadharia na   kinatambulika na Serikali na baada ya kumaliza masoma mwanafunzi ana nafasi kubwa ya kuajiriwa na kujiajiri mwenyewe.

Akizungumza jijini Dar es salaam Julai 05, 2023 Makamu Mkuu wa Chuo hicho anayeshughulikia Taaluma,Tafiti na Ushauri Elekezi Profesa Provident Dimoso alipotembelea banda la Chuo Cha Mipango lililopo katika jengo la Wizara ya Fedha na Mipango kwenye Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF),maarufu Saba Saba, yenye kaulimbiu isemayo"Tanzania Mahali sahihi pa Biashara na Uwekezaji," amesema wanafunzi wa Chuo hicho wanatambuliwa na serikali.

"Chuo hiki ni cha serikali ambacho kipo chini ya Wizara ya Fedha na Mipango, kimesajiliwa na Baraza la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET), na pia kinatambuliwa na Tume ya Vyuo vikuu Tanzania (TCU), pamoja na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB),na hii imekuwa ni kitu chema kwa wanafunzi wetu kupata mikopo,"amesema Prof. Dimoso.

Prof. Dimoso amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa mkopo hiyo ambapo kwa sasa wanafunzi wa Chuo hicho wanasoma vizuri.

Makamu huyo  amesema chuo cha Mipango kimeanzishwa mwaka 1979 na kupewa majukumu makubwa matatu, kutoa Taaluma, kufanya Utafiti, kutoa ushauri Elekezia huku akifafanua kuwa kwa upande wa taalum kimejikita kutoa kozi za muda mrefu na mfupi.

Ameongeza kuwa chuo hicho kinatoa
 kozi za muda  mrefu na mfupi huku akifafanua kwamba kozi zake ni pamoja na Astashahada (certificate),kwa mwaka mmoja, kozi ya diploma mika miwili, degree miaka mitatu na kozi ya Masters degree miaka miwili pamoja na Post graduate diploma mwaka mmoja.
  
Prof.Dimoso ameeleza kuwa kozi zote hizo zinatambuliwa na serikali 
wanafunzi wanapomaliza kozi hizo wanapata umahiri wa kutosha wa  kuajiriwa na serikali au mashirika mbalimbali ya kimataifa.

"Chuo hiki  kina jukumu la kufanya tafiti mbalimbali  na moja ya tafiti tulizofanya hivi karibuni ni tafiti ambayo inahusiana na masuala ya mabadiliko ya tabia nchi pamoja na umasikini," amesema.

Ameongeza kuwa tafiti  hiyo imeonekana wananchi wengi vijijini na zaidi ya asilimia 65 ya watanzania wanaishi vijijini hivyo chuo hicho kinahudumia  watanzania wengi zaidi

Post a Comment

0 Comments

 KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA UTAWALA, KATIBA NA SHERIA YANOLEWA