VETA YAWAKARIBISHA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LAO KATIKA MAONESHO YA SABA SABA

Na Asha Mwakyonde,Dar es salaam

WAZAZI, wananchi wametakiwa kufika katika banda la Mamlaka ya Elimu ya Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA),katika 
Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam(DITF), maarufu Saba Saba, yenye kaulimbiu isemayo "Tanzania Mahali sahihi pa Biashara na Uwekezaji," lengo likiwa ni kujua fursa zinazopatika ili kuwapatia vijana nafasi ya kusomea ujuzi wanaohitaji.

Akizungumza jijini Dar es salaam Julai 03,2023  katika maonesho hayo Mwalimu wa Bidhaa za Ngozi kutoka chuo cha Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA),Dakawa mkoani Morogoro
 Hamidu Mahembe amesema ada ni nafuu ambazo mtu yoyote anaweza kuzimudu kulipa  ambapo kwa kipindi cha miaka miwili  mwanafunzi wakutwa  analipata ya hiyo ya shilingi 60,000 na kukaa bwenini analipata 120,000

Mahembe amesema serikali ndiyo inawasomesha vijana hao kupitia Vyuo vya VETA kwa wale wanafunzi wa muda mrefu.

Amesema kuwa bidhaa za ngozi zimegawanyika katika sehemu mbalimbali zikiwamo viatu, mikoba na mikanda.

Ameongeza kuwa katika Chuo hicho wanatoa mafunzo ya muda mrefu na mfupi kulingana na mteja wao na kwamba kijana akimaliza mafunzo hayo anakuwa na umahiri wa kutengeneza bidhaa hizo za ngozi.

"Wapo vijana wetu waliomaliza Chuo Cha VETA Dakawa wameajiriwa katika viwanda mbalimbali na vikubwa vinavyojulikana kwa uzalishaji wa bidhaa zenye ubora," amesema.

Ameeleza kuwa ujuzi unamkomboa mwanadamu na VETA ipo kwa ajili ya Watanzania ili kupata ujuzi huo wa kuweza kuajiriwa au wa kujiajiri lengo likiwa ni kukuza kipato katika jamii na kwa nchi.

Post a Comment

0 Comments

CHATANDA:RAIS DK. SAMIA AMEIMARISHA SEKTA YA MADINI