Wananchi watakiwa kutumia fursa ya mvua zinazonyesha kupanda miti



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Selemani Jafo akipanda mti katika eneo la Medali ikiwa ni wiki ya upandaji miti.

Na Asha Mwakyonde, Dodoma


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Selemani Jafo amesema matarajio ya serikali ni kupanda miti milioni 276 kwa mwaka na katika kila Halmashauri itatakiwa kupanda miti hiyo milioni 1.5  hivyo Watanzania wanatakiwa kutumia mvua zilizoanza kunyesha kupanda miti.


Pia Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango anatarajiwa kuzindua Sera Mpya 

ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021 katika Maadhimisho ya upandaji miti.


Hayo ameyasema leo wakati wa zoezi la Upandaji wa Miti  eneo la Medeli ikiwa ni wiki la upandaji miti amesema kuwa amefurahishwa na ile kauli "Soma na Mti ambapo wanafunzi wamejitokeza kupanda miti hiyo.


Waziri Jafo ameongeza kuwa serikali imeweka wiki maalumu ya upandaji miti kuanzia Febuari 7 na  kwamba maadhimisho yake yafanyika Februari 12 mwaka huu na kwamba sera mpya ya mazingira ya mwaka 2021 itazinduliwa.


"zoezi la upandaji miti  ndani ya  Taifa letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na nimefarijika sana kuona  wanafunzi kujitoa katika zoezi hili la  kupanda miti," amesema Waziri Jafo


Ameeleza kwamba wanahakikisha  muendelezo wa zoezi  la upandaji miti linaendelea na kuwataka wananchi kutumia mvua kupanda miti ili kuhakikisha Kampeni ya Soma na Mti inafanya vizuri hapa nchini.

Post a Comment

0 Comments

KAMATI YA BUNGE SHERIA YAPONGEZA MAENDELEO YA MATUMIZI YA NeST