WANANCHI DODOMA WAITIKIA AWAMU YA PILI YA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN


 Na Mwandishi wetu,DODOMA 

KATIKA kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma za Msaada wa Kisheria  kwa wakati na Usawa, Wizara ya Katiba na Sheria imeanza kutekeleza rasmi Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia Awamu ya Pili Mkoani Dodoma kwa lengo la kutoa huduma za kisheria na  elimu kwa wanachi wote hasa wale wasiokuwa na uwezo wa kumudu gharama za huduma za Kisheria. 

Katika awamu  ya pili  ya utekelezaji  Wizara ya Katiba na  Sheria na taasisi  mbalimbali katika mnyororo wa haki jinai zinazoshiriki kutekeleza Kampeni hii zitatoa huduma mbalimbali ikiwemo ushauri wa kisheria, utatuzi wa migogoro mbalimbali ikiwemo Migogoro ya Ardhi, Ndola,Mirathi, matunzo ya watoto na masuala ya ukatili wa kijinsia. 

Kampeni ya Msaada  wa Kisheria katika mkoa wa Dodoma inatekelezwa kwa muda wa siku kumi na tano  katika Halmashauri zote nane za Mkoa wa Dodoma zikiwemo  Kata,Mitaa na Vijiji  vyote vilivyopo  katika Halmashauri hiyo bila malipo.



Post a Comment

0 Comments

WANANCHI DODOMA WAITIKIA AWAMU  YA PILI  YA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN